Mathayo 12

1 Wakati huo, Yesu alikuwa anapita katika mashamba ya ngano siku ya Sabato. Basi, wanafunzi wake wakaona njaa, wakaanza kukwanyua masuke ya ngano, wakala punje zake. 2 Mafarisayo walipoona hayo, wakamwambia Yesu, “Tazama, wanafunzi wako wanafanya jambo ambalo si halali siku ya Sabato.” 3 Yesu akawajibu, “Je, hamjasoma alivyofanya Daudi …

Mathayo 11

1 Yesu alipomaliza kuwapa wanafunzi kumi na wawili maagizo, alitoka hapo, akaenda kufundisha na kuhubiri katika miji yao. 2 Yohane mbatizaji akiwa gerezani alipata habari juu ya matendo ya Kristo. Basi, Yohane akawatuma wanafunzi wake, 3 wamwulize: “Je, wewe ni yule anayekuja, au tumngoje mwingine?” 4 Yesu akawajibu, “Nendeni mkamwambie …

Mathayo 10

1 Yesu aliwaita wanafunzi wake kumi na wawili, akawapa uwezo wa kutoa pepo wachafu na kuponya magonjwa na maradhi yote. 2 Majina ya hao mitume kumi na wawili ni haya: wa kwanza ni Simoni aitwae Petro, na Andrea ndugu yake; Yakobo mwana wa Zebedayo, na Yohane ndugu yake; 3 Filipo …

Mathayo 9

1 Yesu alipanda mashua, akavuka ziwa na kufika katika mji wake. 2 Hapo watu walimletea mtu mmoja aliyepooza mwili, amelazwa juu ya kitanda. Yesu alipoona imani yao, akamwambia huyo mtu aliyepooza, “Jipe moyo mwanangu! Umesamehewa dhambi zako.” 3 Baadhi ya walimu wa Sheria wakaanza kufikiri, “Mtu huyu anamkufuru Mungu!” 4 …

Mathayo 8

1 Yesu aliposhuka kutoka mlimani, makundi mengi ya watu yalimfuata. 2 Basi, akaja mtu mmoja mwenye ukoma, akamsujudia akisema, “Bwana, ukitaka, waweza kunitakasa!” 3 Yesu akanyosha mkono wake, akamgusa na kusema, “Nataka! Takasika.” Mara huyo mtu akapona ukoma wake. 4 Kisha Yesu akamwambia, “Sikiliza, usimwambie mtu yeyote, ila nenda ukajionyeshe …

Mathayo 7

1 “Msiwahukumu wengine, msije nanyi mkahukumiwa na Mungu; 2 kwa maana jinsi mnavyowahukumu wengine, ndivyo nanyi mtakavyohukumiwa; na kipimo kilekile mnachotumia kwa wengine ndicho Mungu atakachotumia kwenu. 3 Kwa nini wakiona kibanzi kilicho jichoni mwa ndugu yako, na papo hapo huioni boriti iliyoko jichoni mwako? 4 Au, wawezaje kumwambia ndugu …

Mathayo 6

1 “Jihadharini msije mkafanya matendo yenu mema mbele ya watu kusudi mwonekane nao. La sivyo, Baba yenu aliye mbinguni hatawapeni tuzo. 2 “Basi, unapomsaidia maskini, usijitangaze. Usifanye kama wanafiki wafanyavyo katika masunagogi na njiani ili watu wawasifu. Kweli nawaambieni, hao wamekwisha pata tuzo lao. 3 Lakini wewe unapomsaidia maskini, fanya …

Mathayo 5

1 Yesu alipoyaona makundi ya watu, alipanda mlimani, akaketi. Wanafunzi wake wakamwendea, 2 naye akaanza kuwafundisha: 3 “Heri walio maskini rohoni, maana ufalme wa mbinguni ni wao. 4 Heri walio na huzuni, maana watafarijiwa. 5 Heri walio wapole, maana watairithi nchi. 6 Heri wenye njaa na kiu ya kufanya atakavyo …

Mathayo 4

1 Kisha Roho alimwongoza Yesu mpaka jangwani ili ajaribiwe na Ibilisi. 2 Akafunga siku arubaini mchana na usiku, na mwishowe akaona njaa. 3 Basi, mshawishi akamjia, akamwambia, “Ikiwa wewe ni Mwana wa Mungu, amuru mawe haya yawe mikate.” 4 Yesu akamjibu, “Imeandikwa katika Maandiko Matakatifu: `Binadamu hataishi kwa mikate tu, …

Mathayo 3

1 Siku hizo Yohane Mbatizaji alitokea, akaanza kuhubiri katika jangwa la Yudea: 2 “Tubuni, maana Ufalme wa mbinguni umekaribia.” 3 Huyu Yohane ndiye yule ambaye nabii Isaya alinena juu yake aliposema: “Sauti ya mtu imesikika jangwani: `Mtayarishieni Bwana njia yake, nyoosheni vijia vyake.”` 4 Yohane alivaa vazi lililoshonwa kwa manyoya …