Mathayo 9

1 Yesu alipanda mashua, akavuka ziwa na kufika katika mji wake. 2 Hapo watu walimletea mtu mmoja aliyepooza mwili, amelazwa juu ya kitanda. Yesu alipoona imani yao, akamwambia huyo mtu aliyepooza, “Jipe moyo mwanangu! Umesamehewa dhambi zako.” 3 Baadhi ya walimu wa Sheria wakaanza kufikiri, “Mtu huyu anamkufuru Mungu!” 4 …

Mathayo 8

1 Yesu aliposhuka kutoka mlimani, makundi mengi ya watu yalimfuata. 2 Basi, akaja mtu mmoja mwenye ukoma, akamsujudia akisema, “Bwana, ukitaka, waweza kunitakasa!” 3 Yesu akanyosha mkono wake, akamgusa na kusema, “Nataka! Takasika.” Mara huyo mtu akapona ukoma wake. 4 Kisha Yesu akamwambia, “Sikiliza, usimwambie mtu yeyote, ila nenda ukajionyeshe …

Mathayo 7

1 “Msiwahukumu wengine, msije nanyi mkahukumiwa na Mungu; 2 kwa maana jinsi mnavyowahukumu wengine, ndivyo nanyi mtakavyohukumiwa; na kipimo kilekile mnachotumia kwa wengine ndicho Mungu atakachotumia kwenu. 3 Kwa nini wakiona kibanzi kilicho jichoni mwa ndugu yako, na papo hapo huioni boriti iliyoko jichoni mwako? 4 Au, wawezaje kumwambia ndugu …

Mathayo 6

1 “Jihadharini msije mkafanya matendo yenu mema mbele ya watu kusudi mwonekane nao. La sivyo, Baba yenu aliye mbinguni hatawapeni tuzo. 2 “Basi, unapomsaidia maskini, usijitangaze. Usifanye kama wanafiki wafanyavyo katika masunagogi na njiani ili watu wawasifu. Kweli nawaambieni, hao wamekwisha pata tuzo lao. 3 Lakini wewe unapomsaidia maskini, fanya …

Mathayo 5

1 Yesu alipoyaona makundi ya watu, alipanda mlimani, akaketi. Wanafunzi wake wakamwendea, 2 naye akaanza kuwafundisha: 3 “Heri walio maskini rohoni, maana ufalme wa mbinguni ni wao. 4 Heri walio na huzuni, maana watafarijiwa. 5 Heri walio wapole, maana watairithi nchi. 6 Heri wenye njaa na kiu ya kufanya atakavyo …

Mathayo 4

1 Kisha Roho alimwongoza Yesu mpaka jangwani ili ajaribiwe na Ibilisi. 2 Akafunga siku arubaini mchana na usiku, na mwishowe akaona njaa. 3 Basi, mshawishi akamjia, akamwambia, “Ikiwa wewe ni Mwana wa Mungu, amuru mawe haya yawe mikate.” 4 Yesu akamjibu, “Imeandikwa katika Maandiko Matakatifu: `Binadamu hataishi kwa mikate tu, …

Mathayo 3

1 Siku hizo Yohane Mbatizaji alitokea, akaanza kuhubiri katika jangwa la Yudea: 2 “Tubuni, maana Ufalme wa mbinguni umekaribia.” 3 Huyu Yohane ndiye yule ambaye nabii Isaya alinena juu yake aliposema: “Sauti ya mtu imesikika jangwani: `Mtayarishieni Bwana njia yake, nyoosheni vijia vyake.”` 4 Yohane alivaa vazi lililoshonwa kwa manyoya …

Mathayo 2

1 Yesu alizaliwa mjini Bethlehemu, mkoani Yudea, wakati Herode alipokuwa mfalme. Punde tu baada ya kuzaliwa kwake, wataalamu wa nyota kutoka mashariki walifika Yerusalemu, 2 wakauliza, “Yuko wapi mtoto, Mfalme wa Wayahudi, aliyezaliwa? Tumeiona nyota yake ilipotokea mashariki, tukaja kumwabudu.” 3 Mfalme Herode aliposikia hayo, alifadhaika, yeye pamoja na wakazi …

Mathayo 1

1 Yesu Kristo alikuwa mzawa wa Daudi, mzawa wa Abrahamu. Hii ndiyo orodha ya ukoo wake: 2 Abrahamu alimzaa Isaka, Isaka alimzaa Yakobo, Yakobo alimzaa Yuda na ndugu zake, 3 Yuda alimzaa Faresi na Zera (mama yao alikuwa Tamari), Faresi alimzaa Hesroni, Hesroni alimzaa Rami, 4 Rami alimzaa Aminadabu, Aminadabu …

Marko o 16

1 Baada ya siku ya Sabato, Maria Magdalene, Salome na Maria mama yake Yakobo walinunua manukato ili wakaupake mwili wa Yesu. 2 Basi, alfajiri na mapema siku ya Jumapili, jua lilipoanza kuchomoza, walienda kaburini. 3 Nao wakawa wanaambiana, “Nani atakayetuondolea lile jiwe mlangoni mwa kaburi?” 4 Lakini walipotazama, waliona jiwe …